Mpasuko CCM: Wajumbe Waanzisha Varangati........Rais Kikwete Apokelewa Kwa Wimbo Wa Tuna Imani Na Lowassa.....!!!!.....Tuna Imani na Lowassa

Mambo yamezua jambo ambapo wajumbe wa mkutano wa Halmashauri kuu inayokutana hivisasa chini Rais Dkt Jakaya Kikwete wameonesha wazi kupinga uamuzi wa mbunge wa Monduli Edward Lowassa jina lake kukatwa.

Hayo yamedhihirika hivisasa wakati Mwenyekiti wa chama hicho Rais Dkt Jakaya Kikwete akiingia kufungua mkutano huo ambapo imezoeleka wajumbe huimba kuwa na imani na Mwenyekiti ambaye ni Rais Dkt Jakaya Kikwete lakini leo hali imekuwa tofauti.  Wajumbe walipaza sauti zao wakiimba wimbo wa kuwa na imani na Edward Lowassa.(  Tuna  Imani  na  Lowassa...!!!  Tuna  Imani  na  Lowassa!!)

Mkutano huo  wenye wajumbe  324 kati ya 374 umehudhuriwa na wajumbe mbalimbali wakiwemo baadhi ya wanasiasa walio omba ridhaa ya kuteuliwa kugombea urais ndani ya chama hicho.

Kwa upande  mwingine  mtia nia aliyechujwa Prof. Mark Mwandosya yeye kwa upande wake amewashukuru wananchi kwa ushirikiano walio mpa na kusisitiza kuwa hatogombea tena ubunge katika uchaguzi mkuu ujao.