NAACHA BUKU 15 DAILY NAKUTA UGALI NA DAGAA

Nimevumilia vya kutosha hii tabia sasa naona itakua imefika kikomo. 
Naishi na mpenzi wangu hatujafunga ndoa tatizo nashindwa kumuelewa kila siku niendapo kazini na kurudi jioni lazima nimuachie elfu kumi na tano 15,000/-kusudi nikirudi jioni nikute mezani kumependeza nadhani mmenielewa cha ajabu jamani nakuta ugali na dagaa akibadili sana tembere kaomba kwa jirani.
Huu ni ungwana jamani? kumuambia nashindwa naona kama takua naingilia mambo ya jikoni ambayo hayanihusu na nisipokula huo ugali ananuna.
Sielewi nifanyeje na Nilikuwa nafikiria Kumuoa